GLORY OF CHRIST TANZANIA CHURCH
UFUFUO NA UZIMA KIGOMA
SOMO: MTU WA NDANI_MCHUNGAJI PAUL JOSHUA
TAREHE: 03/12/2017
1Wakorinto 15:40; Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani; lakini fahari yake ya mbinguni ni mbali, na fahari yake ya duniani ni mbali.
 kuna mtu ambaye asili yake ni duniani na kuna mtu ambaye asili yake ni mbinguni; Kuna mwili wa asili ambao ni udongo/mavumbi na kuna mwili wa roho ambao asili ni mbinguni; Kumbe roho inamwili. Mungu ni roho lakini ana macho, ana kinywa, ana masikio, ana miguu; unavyoona jinsi mwili wa nyama ulivyo na vingo ndivyo na mwili wa roho ulivyo. Wachawi wanapotaka kumshambulia mtu hawaangalii mwili wako wa nje ila huangalia ndani, wewe ninani. Sasa mtu wa ndani anatakiwa afanye kazi, ashinde maana ndiye ana kila kitu chako. Mungu anaweka baraka kwenye kiungo cha mtu. Kuna mtu akiongea tu ni kama mtu aliye soma sana wakati elimu yake ni darasa la saba; ni kwakuwa baraka zake ziko kinywani.
Maskio; mtu aliye barikiwa masikio ya rohoni atasikia kila kitu hata kama hayupo eneo husika (anapata raarifa zote za rohoni). Kuna watu ni viziwi wa rohoni, hawawezi kusikia chochote hata kama atazungumziwa hali na yeye yupo. Wachawi wakijua unasikia wakiwa wanafanya vikao vyao (kwa sababu una masikio ya rohoni) wataanza kukuwinda ili kufanya vita na wewe. Ukiwa muombaji halafu unamasikio, una macho na unakinywa, unauwa wachawi wote. Masikio ya rohoni yakichukuliwa unakuwa kiziwi wa rohoni.
Sura; Ni kumpa mtu kibali mbele za watu. Kuna mtu anaweza kuwa wa kawaida tu lakini sura yake ya ndani ikawa imebarikwa; hivyo utaona anapata kibali sehemu  nzuri usiyo dhania. Kuna soko la kimataifa la kuuza nyota za viungo vya binadamu, Viungo vya mwili mmoja vinaweza kugawanywa kwa watu hata zaidi ya kumi; Utakuta akili anauziwa mtu mwingine, nywele, kucha, macho, masikio, miguu, mikono, na vinginevyo vingi.  Ufunuo 18:11 Hawa ni wafanya biashara wa nchi/dunia, ni biashara ambayo wanauza viungo vya miili na roho za binadamu. Mtu unapoenda kwa mganaga wa kienyeji kutafuta kibali au nyota ya maisha, ukweli  ni kwamba, mganga wa kienyeji yeye kama yeye hana kitu chochote cha kukupa wewe bali huchukuwa viungo vya rohoni kutoka  kwa mtu/ watu tofauti tofauti na kukupachikia wewe.
Kinywa;(Kinywa cha rohoni) Mungu aweza kuweka Baraka kwenye kinywa cha mtu. Mutu ataweza kuongea na mtu yeyote. Kuna  mtu alikuwa anatumiwa kuongea sehemu mbali mbali hata kwa kukodiwa ili aongee kwa niaba ya wahusika kwani maneno yake yalikubalika  kila alipoongea; na hivi leo  mtu huyo anaonekana pumba aongeapo kwani kinywa chake cha rohoni hakipo tena, kimeshachukuliwa na wafanya biashara wa viungo vya miili na roho za binadamu kuuzia watu wengine. Utakuta mtu mwingine anaongea matusi, kusengenya wengine tangu asubuhi mpaka jioni kwasababu hana mdomo wa kuonelea na si kwamba anapenda la, anatamani sana kuongea mazuri ila kinywa chake hana, kinatumika na mtu mwingine na huyo mtu anaye tumia kinywa cha mtu huyo utaona hata akiimba au akiongea neno lisilo maana yoyote, atakupalika sana kwani kinywa anachotumia ni kinywa chenye kibali. Pia kuna kinywa chenye nguvu; Mtu mwenye kinywa chenye nguvu akitamka jambo lolote kuwa leo  litatokea, na inakuwa hivyo kwa sababu kinywa chake ni chenye nguvu na mamlka. Kinywa kinaweza kufungwa au kuchukuliwa na wachawi, utakuta mtu anabiashara ila anashindwa/hawezi kuongea na mteja kumshawishi anunue.  Kinywa kina ambatana na ujasiri. Kuna siri kwenye kinywa, kama huna ujasiri huwezi kuongea na mtu yeyote hata kama yeye anahitaji aongee na wewe; na watu wengi wamechukuliwa kinywa. Wachawi/waganga wanaweza kuchukua kinywa. Ukiwa na kinywa cha rohoni:- Unaweza kuongea na mtu yeyote, Unaweza kuomba chochote kwasabau unanguvu na mamlaka kwenye kinywa.
Tumbo: Kuna matumbo ya kiroho; Mungu anaweza kubariki tumbo lako, Utakuta Mungu alikuchagua akaribariki tumbo lako kuzaa viongozi wa nchi, wachungaji, watoto wazuri; Lakini wachawi wakaliona hilo tumbo mapema hivyo wakalichukuwa na hivi leo analitumia mwingine na wewe huku unazaa watoto wa ajabu au hakuna kabisa kwani hauna tumbo la uzazi. Wewe uliyepata neema ya kuyafahamu haya, chukua hatua mapema kurudisha kila kiungo cha mwili wako kilichochukuliwa na wafanya biashara wa viungo vya miili ya wanadamu katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Amen!

DAMU JUU YA SHERIA



GROLY OF CHRIST TANZANIA CHURCH
UFUFUO NA UZIMA - KIGOMA,
SOMO: DAMU JUU YA SHERIA, 
AP: MORIS
TAREHE 12/11/2017.
WAEBRANIA 9:22 Hii ni damu ya agano mlioamuriwa na Mungu,na ile hema nayo na vyombo vyote vya Ibada alivinyunyuzia damu vivyo hivyo,na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu na pasipo damu kumwagwa hakuna ondoleo, mtume Paulo anazungumza na waebrania kwamba waitumie damu ya Yesu kwenye maisha yao kama agano waliloamuriwa na Mungu na kupitia hii damu inasamehe dhambi, inaponya magonjwa na kuwa upatanisho kati ya Mungu na Mwanadamu.
Damu ya Yesu ni daraja kati ya Mungu na Mwanadamu, unapoitumia damu ya Yesu magonjwa yanatoweka. Damu ya Yesu kuna wakati inaitwa damu ya mwana kondoo ndio maana tunajifunza kwamba tunaweza kuwashinda mashujaa wa dunia kwa Damu ya Yesu na kwa neno la ushuhuda, sdamu hii inaweka upatanisho na kuwaweka pamoja na Mungu na mwanadamu, ndio mana kama mkristo unahitaji kuitumia sana hii damu ya Yesu kristo maana inatenda kazi jana leo na hata milele.
Shetani nae hutumia damu ili kuyaharibu maisha ya watu, kupitia mawakala wake kama waganga, wachawi, na wasoma nyota; wanaweza kutumia damu ili kuchafua maisha ya mtu. Maisha ya mtu yanaweza kuchafuka kwa ama kusafishwa kwa damu, wachawi wanaweza kuitumia damu na wakafanikiwa katika mambo yao kwa sababu ni sheria ya rohoni. damu ni uhai, kuna vitu ambavyo damu imevibeb; Imeandikwa, kushindana kwetu si juu ya damu na nyama, kumbe damu inaunganisha mwili na Roho na kutenda kazi na kuyatimiza makusudi yake.
Damu inatakasa, inapatanisha, inatetea, inalinda, ni daraja kati ya Mungu na mwanadamu ndio mana tunaitumia damu ya Yesu kunyamanzisha kila damu inayoongea mabaya kwenye maisha yetu; kama ni damu ya mwanadamu, damu ya kuku, damu ya kondoo ama ya ngombe tunanyamanzisha kila damu kwa damu ya Yesu kristo.
Ili maisha yako yafanikiwe na yainuliwe yanahitaji damu ya Yesu, huwezi kushinda pasipo damu ya Yesu na kwa damu hii tunabatilisha kila damu za waganga na za wachawi waliofunga maisha yetu kwa damu ya Yesu. Amina.
SOMO LA LEO 15/10/2017,
SNP:PAUL JOSHUA,
KIFUNGO CHA MAUTI.
Mauti ni kifo,
ZBURI 102:20. Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa, na kuwafungua walioandikiwa kufa. Mungu huwafungua waliondikiwa kufa, kuna watu wengine wameandikiwa kufa. Mtu anaugua lakini unakuta ameandikiwa kufa, ugonjwa huo ni ugonjwa kwaajili ya kuleta mauti. Unaona mtu anaugua malaria isiyo isha lakini mwisho wake ni kifo, ama typhoid lakini mwisho wake ni kifo, lakini zaidi yoyote adui anaweza kukufunga kwenye magonjwa, unajiona unamagonjwa na unatumia pesa zote kutibu magonjwa hayo na mwisho ya yote unakupeleka kwenye mauti. Kuna ufungwa wa rohoni kama ilivyo kwa wafungwa wa gerezani, wamefungwa lakini kila mtu anahukumu yake. Hivyo hivyo mtu amefungwa na matatizo mengi lakini ameandikiwa hukumu na hukumu hiyo inaweza kuwa ya mauti.
Shetani na mawakala wake wanaweza kuifunga familia. Wanaweza kufunga watoto, ndoa, uchumi ama kazi.
MITHALI 24:11 uwaokoe wanaochukuliwa ili wauwawe nao walio tayari kuchinjwa uwaokoe.
Kuna watu waliochukuliwa kama wafungwa lakini mwisho wake ni kuuawa. Unaweza kufungwa na aliyekufunga hujui alimaanisha nini kukufunga. Na mara nyingi tatizo linaanza kidogo, maana shetani huanza kidogo kidogo na baadae anafanya tatizo linakuwa kubwa na hatimae anakumaliza.
ISAYA 42:7 kuyafunua macho ya vipofu, kuwatoa gerezani waliofungwa, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufungwa.
Ni nyumba ya mtu lakini inatumika kufunga, ni gereza. Kwaniwa wachawi wanafunga maisha yako, wanaona nyota yako na hatima ya maisha yako nao wanakufunga. Unakuta mtu anamaisha magumu, lakini akifunguliwa tu hata maisha yake yanabadilika.
LUKA 13:10-16… na huyu mwanamke aliyeuzao wa Ibrahimu ambaye shetani amemfunga miaka kumi na minane hii, haikupasa afunguliwe kifungo hiki siku ya sabato.
Shetani anaweza kumfunga mtu asifanikiwe, wachawi wanaweza kukufunga usizae au usifanikiwe. Lakini Yesu hatakuacha kwenye vifungo hivyo.
Yusuphu alizingiziwa amembaka mke wa mfalme lakini bado Yusuphu alikuwa amebeba kusudi la Mungu ndani yake,ndio mana hakumwacha waLa kumpungukia hata ndani ya gereza bado Mungu alikuwa pamoja nae,Mungu wetu si Mungu wa hasara Mungu wetu ni Mung wa faida,ni bora aangamize watu lakini kusudi lake libaki limesimama.
Kuna kitu Mungu alikupa ambalo kupitia hicho Mungu atakutoa ndani ya Gereza,Yusuphu amekaa gerezai na wafungwa wenzio badae wakaota ndoto lakini ndoto zikawachanganya,Mungu akamuandaa yusuphu kuwa jibu la ndoto zao zilizowachanganya,akawambia mana ya ndoto zao,badae Mfalme nae akaota ndoto ikamchanganya sana akawaita wachawi,waganga,wasoma nyota wote hawakufanikiwa,badae akaitwa Yusuphu akatafsiri ndoto ya Mfalme badae akatolewa gerezani na kuwa waziri mkuu,Mungu alimuinua yusuphu kwa kile alichompa ndani yake ndicho kilicho mtoa gerezani,na kupita karama hio Mungu aliompa akamuinua.Alianza kama mfungwa lakini akamaliza mwenye heshima,na kuwasidia ndugu zake kupitia kile Mungu alichoweka ndani yake.
Kusudi la Mungu kwenye maisha yako ndilo litakalo kutoa kwenye shida unayopitia leo,lakini shetani anafanya njia ya kukuonesha kwamba huwezi kutoka hapo ulipo lakini nakwambia Mwana wa Mungu kwamba mwenye Mungu mpe mda tu,Mungu atamuinua
MAMBO YA WALAWI 19:26 Msile kitu chochote pamoja na damu yake,wala msifanye kuroga wala kutumia utambuzi,kumbe mtu anaweza kurogwa na wachawi,waganga, wasoma nyota ili usifanikiwe,usiolewe,usizae,wala usifanikiwe kwenye maisha yako,lakini leo mtu wa Mungu unatoka na Mungu akikutoa hapo watu watakushangaa,mana hata kuacha kama ulivyo.
ZABURI 18:4 Kamba za mauti zilinizunguka, mafuliko ya uovu yakanitia hofu,kamba za mauti zilinizunguka na mitego ya mauti ilinikabiri,kuna watu wamefungwa na kamba za Mauti umetumia kaili zako na ngvu zako lakini imeshindikana kwa sababu aliekufunga alimaanisha kukufunga na alitoa sadaka,na mwisho wake alikdhamilia ni kifo,lakini kile ambacho Mungu amepanda ndani yako ndicho kitakacho kuponya ili kusudi la Mungu litimizwe,ni maombi yangu mchana wa leo Mungu kausogeree pale ulipo ili akuponye aiponye ndoa yako,biashara yako,kazi yako na familia yako kwa ujumla.
Wakati mwingine Mungu anaruhusu upitie kwenye hali Fulani ya tatizo ili ujifunze,na badae uwe mwalimu wa wengine,usiogope kwa yale unayopitia leo Mungu anakusaidia leo.

 
 
 

SOMO: UZAO ULIOLAANIWA

“UZAO ULIOLAANIWA”
SNP-PAUL JOSHUA
JUMAPILI YA TAREHE 7/8/2016
Watu wengi wana mateso lakini mateso hayo asilimia kubwa yameanzia kwenye asili ya kwao, kuna wengine wana asili ya mwanza,kibondo, kigoma, kasulu, manyovu nk. Ukifuatilia mateso mengi ambayo unapitia kwenye familia kuna mtu ambaye alipitia matatizo hayo kwenye familia. Kama kuna mtu ana matatizo Fulani yanaweza kutembea kwenye familia kizazi hadi kizazi.
MWANZO 12:1 BWANA akamwambia Abrahamu, Toka wewe katika nchi yako na jamaa zako, na nyumba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha. Nami nitakufanya kuwa Taifa kubwa na kukubariki na kulikuza jina lako nawe uwe Baraka. Nami nitawabariki wakubarikio naye akulaaniye nitamlaani, na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.
Mungu anamtenga Ibrahimu na ndugu zake wote ili afanye agizo nay eye, Mungu alikuwa anaandaa mazingira ili Yesu azaliwe kwenye uzao wa Ibrahimu.
MATHAYO 1:1 Kitabu cha ukoo wa Yesu kristo, mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.
Mungu akitaka kukubariki cha kwanza ni lazima akutenge na mauzauza ya ukoo, akutenge na dhambi ndio maana Mungu akumtoa Ibrahimu ili aende kwenye nchi nyingine.
Mungu akaanza ukoo mpya wa Ibrahimu, ukoo uliojitenga na ukoo wenye wachawi, magonjwa, laana. Mungu anaweza kulikuza jina lako hata kama umezaliwa kijijini, utajulikana maeneo yote, kumbe jina linaweza kukuzwa ulianza chini kwenye magonjwa, ulianza kwenye shida lakini BWANA akilikuza jina utamaliza mwenye heshima; kama Mungu alivyolikuza jina la Ibrahimu leo hii linajulikana kwenye mataifa yote.
Mwanzo wako siyo mwisho wako, kuanza vibaya haimaanishi kwamba utamaliza vibaya, wale walio kuzalau watakushangaa umefanikiwaje na kila mmoja atasema huyu ni ndugu yangu, hata Yule aliyekuloga atasema ni ndugu yangu, hata Yule aliyekutema mate atasema huyu ni ndugu yangu kwa maana BWANA atalikuza jina lako.
Mungu Mungu alianzisha uzao mpya wa Ibrahimu na akaweka agano naye akimwambia mataifa yote watabarikiwa kupitia yeye.
Kumbe Baraka yaweza kutembea uzao hadi uzao na ikasambaa kwenye uzao wote, kama vile Baraka ya Ibrahimu ipo hadi leo tumebarikiwa.
Na laana inaweza kutembea uzao hadi uzao unajikuta unapitia mateso, na magonjwa, mikosi laana, balaa, umaskini; kumbe yametoka kwenye familia yenu. unaweza ukawa kuna shida unapita ambayo imetokea kweye ukoo na imekuwa ikitembea kizazi hadi kizazi.
Mtu anaweza kurithi tatizo, anakuwa anasumbuliwa na magonjwa ambayo yameanzia kwao, kuna mtu mwingine ni kweli ameokoka lakini kuna vitu vinamsumbua ambavyo vimeanzia kwenye ukoo.
Kuna watu wengine wana vitu ambavyo waliachiwa na wazee wao ambavyo vinawatesa kwenye maisha yao; kuna kitu ambacho hukipendi kwenye maisha yako lakini kimekuja kutoka kwenye familia yenu, na leo tunakivunja kwa jina la Yesu.
Kama Baraka zinaweza kutembea kizazi hadi kizazi, hivyo hivyo na laana nazo zinaweza kutembea kizazi hadi kizazi. Kuna wengine wanajikuta wana roho za kuolewa na kuachika, shida inakuwa siyo wewe wala shida siyo mwanaume ila shida inakuwa imeanzia kwenye familia. Unaweza kurithi matatizo, magonjwa, laana, umaskini, roho ya kuoa na kuacha ambayo ukifuatilia inakuwa ilianzia kwa babu.
Kuna wengine wanajikuta wana roho ya kutokusoma maana mizimu inasema kwenye ukoo huu hakuna aliyesoma wewe unataka usome unaenda wapi; lakini leo nakutangazia familia yenu itakuwa wa kwanza kusoma shule. Watu mnakuwa mnaakili darasani lakini mnaishia njiani, mnatamani kusonga mbele lakini unashindwa shida inakuwa siyo wewe ila umezaliwa kwenye ukoo tata. Kazi inakuwa ni kutoka kuiponyoka mizimu na mashetani, na ukifanikiwa kutoka umefanikiwa.
Kuna wengine kwao kuna roho ya kifo, wanakuwa kila mwaka ni lazima wazike mtu ingawa wengine wanakuwa wameokoka. Huyo anakuwa ni shetani ambaye alikabidhiwa ukoo kwa masharti kila mwaka apewe mtu.
Kuna kitu ambacho familia imekwisha kukipokea kutoka kwenye familia, ambacho ni roho tayari wameshaipokea itakayotesa familia kwakuwa ni urithi kutoka kwenye ukoo.
Kwenye familia kunakuwa hakuna aliyefanikiwa sasa wewe unapojaribu kupiga hatua mizimu inakushikilia na kukurudisha nyuma kwa sababu kwenye ukoo wenu hakuna aliyefanikiwa, hakuna aliyejenga nyumba, hakuna aliyenunua hata Tv, hakuna hata aliyesoma shule, wala hakuna aliyewahi kuwa mchungaji.
Kuna familia zingine kuna wakala wa shetani ambaye anafanya biashara inakuwa kila anayezaliwa kwenye familia anauzwa kwa wachawi, mtu ambaye amezaliwa ana kitu anauzwa, anauza matumba ya uzazi anafanya biashara ya kuuza watu.
Yale ambayo unapita leo na wanao watapitia kama usipovunja na kuharibu.
ISAYA 57:3 Lakini ninyi karibuni hapa, enyi wana wa mwanamkwe mchawi, uzao wa mzinzi na kahaba.
Huu ni uzao ambao kuanzia babu alikuwa mzinzi, na hii inakuwa ni roho inatembea kwenye familia inatembea hadi kwenye familia. Ama familia hii inakuwa kuanzia bibi alikkuwa kahaba sasa roho hii inaendelea kwenye familia kwa wajukuu hadi kwa vitukuu. Ama uzao mwingine ni wa wachawi maana yake babu anapokaribia kufa anamchagua mtu wa kumrithisha uchawi wake.
Leo ni siku ya kuwafungua wote ambao wamefungwa na mizimu ya familia wamekuwa na magonjwa ya kurithi, laana za ukoo na mikosi, tunavunja kila balaa zilizotoka kwenye familia kwa jina la Yesu.
LikeShow more reactions

KESHO ILYOPINDISHWA

UFUFUO NA UZIMA KIGOMA

JUMAPILI TAR 15/5/2016
SOMO: KESHO ILIYOPINDISHWA
SNP: PAUL JOSHUA
Mungu anapomuumba mtu anampa mwanzo wake na mwisho wake. Anampa aanzie maisha ya chini lakini hatima yake iwe maisha mazuri anaweza akaanza na nyumba ya udongo hatima yake akamiliki gorofani, anaweza akaanzia kwenye magonjwa lakini kesho yake ni uzima, anaweza akawa masikini lakini hatima yake ni kumiliki utajili. Lakini shetani huwa anaweza kuiona kesho au hatima ya mtu na aakamua kuipindisha ili kesho yake ambayo anatakiwa amiliki isitimie, lakini lleo tunawatangazia wachawi wote tunawashinda kwa damu ya mwana kondoo.

WARUMI 8:29-30 Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua  tangu asili wafananishwe na mfano wa mwana wake ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi; na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita na wale aliowaita akawahesabia haki na hao aliowahesabia haki akawatukuza.
Mungu alikuchagua tangu mbinguni uwe mtu fulani, uwe mchungaji, uwe tajiri, uwe na ndoa nzuri uwe na maisha mazuri; Mungu alikuchagua tangu asili, lakini shetani anapambana na kile ambacho Mungu alikipanga juu ya maisha yako. Shetani anaangalia mtu huyu amezaliwa lakini miaka hamsini au thelasini ijayo mbele atakuwa mtu Fulani;  ni kweli amezaliwa kijijini lakini mwisho wake ni kuishi marekani hakikisheni mnapindisha maisha yake aishie kwenye magonjwa. 

Wanasoma nyota yako na kujua Mungu amekupangia nini ni kweli ana kasi ya kumtumikia Mungu, hakikisheni mnamfunga; Lakini leo tunawatangazia wachawi wote kwamba tumepewa nguvu ya kushinda kwa jina la Yesu. Tunaye Yesu ambaye alishinda kifo na mauti, yawezekana ulianza kwa huzuni lakini utamaliza kwa kucheka hata Yesu alizaliwa kwenye nyumba ya fundi selemara lakini akaishia kuwa mfalme wa wafalme. Mungu huwa anaiandaa kesho ya mtu, na anapokuokoa lengo la kwanza la Mungu ni kumpeleka kwenye hatima ya maisha mazuri, hata kama ameanza vibaya lakini atamaliza vizuri kwa jina la Yesu.

AYUBU 8:5-7 Wewe ukimtafuta Mungu kwa bidii, na kumsihi huyo mwenyezi ukiwa wewe u safi na mwelekevu; hakika yeye sasa angeamka kwa ajili yako na kufanya makazi ya haki yako kufanikiwa. Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo, lakini mwisho wako ungeongezeka sana.
Hata kama umeanza vibaya mwanzo wako umekuwa sio mzuri lakini BWANA anakuja kufanya makazi kufanikisha haki yako na hatima yako inaongezwa, kesho yako inakwenda kufanikiwa ule uchawi ulifanywa ju yako ili kupindisha kesho yako ili wakuingize kwenye huzuni tunaubomoa kwa jina la Yesu.

MATHAYO 2:1-2 Yesu alipozaliwa katika Bethlelehemu ya uyahudi, zamani za mfalme Herode tazama mamajusi wa mashariki walifika yerusalemu wakisema. Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa wayahudi? Kwa maana tuliona nyota yake mashariki nasi tumekuja kumsujudia.
Mamajusi hawakupigiwa simu bali waliiona nyota ya Yesu wakajua kuwa huyu ni mfalme amezaliwa; wakaenda kumsujudia akiwa bado mchanga fedha zikaanza kuja, dhahabu zikaanza kuja, zawadi zikaanza kuja kumbe nyota iking’aa fedha zinakuja, zawadi zinakuja, dhahabu zinakuja nyota yako ing’ae leo kwa jina la Yesu.
Nyota ya Yesu ikaonekana akiwa mchanga, ingawa alizaliwa kwenye holi la ng’ombe lakini hatima yake akaishia kuwa mfalme; hata wewe usikate tama kwenye maisha yako nyota yako inangaa tena haijalishi umepitia nini kwenye maisha yako ingawa ulisoma shule bila hata viatu, au hata shule hujasoma lakini Mungu anakuinua tena kwa jina la Yesu.

Tunawatangazia adui zako ipo njia nyingine hata kama ulifeli mtihani, ipo njia nyingine hata kama hujasoma sana ipo njia nyingene ambayo haihitaji uwe umesoma sana bali inamhitaji roho mtakatifu. Yesu yupo kwaajili yako usivunjike moyo mwambie Yesu akuonyeshe njia ya kupita; yawezekana mchumba wako ulimsubili kwa muda wa miaka mingi lakini sasa amekwambia amepata mwingine, usiwe na wasiwasi mtazame Yesu. kila jambo lina kusudi la Mungu hata kama unapitia mateso ingawa Ayubu alipitia mateso lakini hakupenda apitie mateso, ndani ya mateso ya Ayubu kulikuwa na kusudi la Mungu.
Heri wewe unayekula ugali kwa tembele kila siku lakini nyumba yako ina amani kuliko nyumba ambayo wanakula pilau na kuku kila siku siku lakini nyumbani ni ngumi kila siku.

Kuna watu wengine wamepindishwa kona, wanajikuta wanafanya kazi ambayo siyo ya kwao mtu anajikuta alipanga awe Rubani lakini anaishia kuwa mama wa nyumbani, alitakiwa awe mbunge lakini anaishia  kuwa mpiga bodaboda na shetani amepindisha maisha ya watu kwa sababu aliona nyota zao. Wachawi wapo wanaweza kumloga mtu asisome shule, asizae watoto, asipate kazi wanapindisha kesho ya mtu na anajikuta anaishia kufanya kazi ambayo haipendi.
Kuna watu wengine kesho yao ilipindishwa kwa namna ya kupewa uchawi wakiwa wadogo au wakubwa, wengine wamejikuta wanaitwa wachawi ingawa hawalogi, wengine kuna kitu ambacho walipewa nyumbani kwenu yawezekana madawa, mahirizi yamebaki yanakutesa kwenye masha yako na mwisho wake yatakumaliza mwenyewe; kesho inakuwa imepindishwa hauwezi kufikia malengo ambayo Mungu aliyapanga kwenye maisha yako. Watoto wengine hatima ya maisha yao imepindishwa walitakiwa wawe shule lakini wanaishia kuloga, wengine walitakiwa wasonge mbele kwenye maisha yao yakini wanaishia kuloga.
Kuna mwingine alitakiwa awe muimbaji lakini kesho yake imepindishe, mwinginge alitakiwa afanye biashara kesho yake imepindishwa anajikuta anapitia maisha magumu ni kwa sababu wachawi waliona kesho yako, waliona hatima ya maisha yake wakaamua kuipindisha, lakini leo tunaangusha falme zao kwa jina la Yesu.



SOMO: VIFO VYA KUTENGENEZA

SOMO: VIFO VYA KUTENGENEZA
SNP: PAUL JOSHUA
Ni kweli watu wanakufa na kuna vifo ambavyo ni mpango wa Mungu lakini kuna asilimia kubwa ya watu ambao wanaokufa; na vifo hivyo vinakuwa ni vifo vya kutengeneza. Mtu anapozaliwa Mungu anampa miaka mingi ya kuishi lakini hapa katikati wachawi wanatokea wanatengeneza matukio ili kufupisha maisha yako. Yawezekana umetengenezewa kifo kwenye ukoo wako au kwenye familia yako na kabla hakijakupata leo tunaibomoa kwa jina la Yesu.

MATHAYO 27:1 Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote wa wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu wapate kumwua.

Tunaona kikao cha wazee kinaandaa mauti juu ya Yesu, kumbe watu wanaweza kukukalia kikao ama usiku ama mchana wakaandaa kifo kwenye maisha yako. kwa maana kila tukio baya linalokutokea wewe kuna sehemu limetokea hakuna tukio linakuja kwako kwa bahati mbaya. Matukio yote mabaya yanatengenezwa kuzimu, na mazuri yanatengenezwa mbinguni; na leo tunaamuru mbingu itengeneze mambo mazuri kwaajili yako, kwaajili ya familia yako kwa jina la Yesu.
Wazee wakaona kati ya wanafunza kumi na mbili wa Yesu kuna mtu ambaye watamtumia ili kumwangamiza Yesu, Yuda akaitwa akaambiwa unataka shilingi ngapi akasema nataka vipande ishirini vya fedha.

Kuna kundi la watu wamekaa kikao ili kutengeneza kifo kwaajili yako lakini leo kabla hujalia wewe watalia wenyewe. Maana Yuda aliyemsaliti Yesu kabla Yesu hajafa Yuda akajinyonga, msalaba ambao aliuandaa Hamani ili kumtundika Morkedai akatundikwa yeye; na leo kila aliyekaa kikao kuandaa kifo juu ya maisha yako kiwarudie wenyewe; maana imeandikwa anayepolomosha jiwe kwaajili yako limrudie mwenyewe, anayekuchimbia shimo atatumbukia mwenyewe.

UKiri: Kwa damu ya Yesu ninabomoa kila uchawi uliotumwa kwenye familia yangu roho za kifo ninazibomoa kwa jina la Yesu, hakuna kifo kwenye familia yangu, kwenye nyumba yangu, kwenye ndoa yangu, kwa watoto wangu, ninakataa kwa jina la Yesu.
Adui zako waache waje maana wanakutengenezea mafaninikio, ili ushindi uje kwenye maisha yako ni lazima Yuda awepo ili akutengenezee mazingira uinuke. Yule adui yako ni daraja la ndoa yako, ni daraja la huduma yako, na ukimuona adui yako mwambie wewe ni daraja langu bila wewe sitaweza kupiti.

Usiogope kwaajili yao kwa maana wao wanataja magari, wao wanataja farasi, wao wanataja waganga wa kienyeji, lakini sisi tunalitaja jina la BWANA. Ni kweli wanashindana nasi lakini hawatashinda maana walio upande wetu ni wengi sana kuliko walio upande wa adui zako.
Anayeaandaa kikao kwaajili yako ni daraja la maisha yako bila yeye huwezi kupita, wamekaa vikao wanajadili utakufa lini? Imeandikwa Sitakufa bali nitaishi hadi niyasimulie matendo makuu ya BWANA hautakufa kwa damu ya mwana kondoo.
Inawezekana kuna wazee wa mtaa wamekaa sehemu ili kujadili ndoa yako, kujadili masomo yako, kujadili kazi yako, lakini imeandikwa vita si vyako bali ni vya BWANA nyamazeni kimya muone BWANA atakavyowapigania wamisri mnaowaona leo hamtawaona tena maadui zako walioinuka leo hutawaona tena.

Kifo kinaweza kutengenezwa kwa njia ya ajali; kwa maana hakuna dereva anayependa kufa, au hakuna bodaboda anayependa kufa hata kama ni mlevi. Lakini wachawi wanaweza kutengeneza kifo cha ajali; wanaweza wakaita majini jini makata, jini subiani, wanatoa kafara ya damu wanayapa majini wanayaambia kaa barabarani ili mtu Fulani anapokuja umtie kizungu-zungu anguke.
Kifo kinaweza kutengenezwa kwa namna ya magonjwa. Kuna kiwanda sehemu cha kutengeneza magonjwa, na ukitaka kutoka kwenye magonjwa tafuta kiwanda cha kutengeneza magonjwa, maana siyo kila mwenyeugonjwa ni wa kawaida,siyo kila Ukimwi ni wa kawaida, unaweza kutengenezewa. Unaweza ukaenda kupima ukaambiwa una sukari au unaambiwa moyo umepanuka kumbe yanakuwa ni magonjwa ya kutengeneza.
Hata kwenye familia mnaweza kutengenezewa magonjwa unakuta kila mwaka lazima afe mtu, wengine unakuta kwenye familia kuna ugonjwa wa presha, ugonjwa wa moyo, sasa leo kile kifo ambacho kimetengenezwa kikupate, wewe au familia yako au watoto wako tunakibomoa kwa jina la Yesu.

DANIEL 6:1-7 Ilimpendeza Dario kuweka juu ya ufalme maliwali mia na ishirini, wawe juu ya ufalme wote na juu yao akaweka wakubwa watatu, na Danieli alikuwa mmoja wao, ili maliwalo hao watoe hesabu kwao mfalme asipate hasara. Basi Danieli huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwakuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote. Basi mawaziri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danieli kwa habari za mambo ya ufalme lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu wala hakuonekana kosa wala hatia ndani yake. Ndipo wale watu wakasema hatutapata sababu ya kumshitaki Danieli huyo tusipoipata katika sheria ya mambo ya Mungu wake. Basi wale mawaziri na maamiri wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme wakamwambia hivi mfalme Dario uishi milele. Mawaziri wote wa ufalme na manaibu na maamiri na madiwani na maliwali wamefanya shauri pamoja ili kuweka amri ya kifalme na kupiga marufuku ya kwamba mtu yeyote atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote au kwa mtu awaye yote katika muda wa siku thelasini ila kwako Ee mfalme atatupwa katika tundu la simba.
Tunawaona hawa walifanya shauri kwaajili ya Danieli ili kuandaa kifo kwaajili yake, muda mwingine inawezekana Mungu amekuinua mahali pako pa kazi adui zako wanaamua kufanya shauri ni jinsi gani wakuangamize. Lakini usiogope Mungu yuko pamoja nawe hakuna jambo lisilowezekana kwake, watafanya sana mashauri lakini hayatafanikiwa kwa jina la Yesu.
Usiogope adui zako wewe songa mbele utafanikiwa mbele ya macho yao; adui yako ni daraja lako na ukitaka upite tafuta adui, ukimuona adui amekuja kwako ujue kuna hatua nyingine kwenye maisha yako. Hao wamisri unaowaona leo hautawaona tena maana BWANA atakupigania f-Farasi na mpanda Farasi BWANA amewatosa baharini, leo adui zako tunawatosa ziwa Tanganyika kwa jina la Yesu.

Unapoona jambo limekutokea iwe kwenye ndoa ama kwenye huduma kuna sehemu kikao kimekaliwa, tafuta kikao kilipokaliwa usihangaike na magonjwa tafuta kiwanda cha magonjwa tunazifuata kwenye ulimwengu wa roho na kukipasua kwa jina la Yesu.
Kunapokuwa na watu wanakutafuta lazima Yuda awepo, mtu anayekujua vizuri ni lazima awepo ili kuwaambia latiba zako huwa zinaendaje, anakuwa anakujua unatoka saa ngapi na unarudi saa ngapi na unapita njia ipi, lakini leo tunatuma malaika kwenye kila hatua zako wakutangulie unapopanda gari na kila unapokanyaga nyayo za miguu yako. Wanatega mitego mauti ikupate popote ulipo siyo wewe tu hata wanao lakini kwakuwa umeokoka neema yako yatosha kuwafunika ndugu zako na watoto wako hata kama hawajaokoka.

Dalili za kujua kama kuna roho ya kifo au mauti imetumwa kwako, au kwenye familia yako.
1. Kuota ndoto za msiba; tambua kuna jambo baya ambalo limetumwa lije kwenye maisha yako au kwenye familia yako.
2. Kuota unalia; tambua kuja jambo baya limepangwa lije likulize.
3. Kukosa amani; yaani siku nzima hauna amani, unalala usingizi unaota ndoto mabaya, unashangaa mbona sina amani leo hiyo ni ishara kuna roho ya kofo ama kwenye familia.
4. Moyo kushituka-shituka. Unatembea unawaza kifo, Ndio maana mtu aliyeokoka mmoja anaweza kuzuia mauti kwenye familia nzima.
Ukiri: kwa damu ya Yesu roho ya kifo iliyotumwa kwangu au kwenye familia yangu ninaivunja kwa jina la Yesu, nakataa kifo kwenye maisha yangu kwa jina la Yesu, nakataa kifo kwenye familia yangu, kwenye ukoo naibomoa roho ya kifo kwa jina la yesu.